Aliagiza wakuu wa upelelezi wa mikoa na mawakili wafawidhi wa Serikali, kukaa kwenye meza moja na kujadili namna ya kurudisha utaratibu huo.
“Kufanya hivyo ni kuipigia saluti Serikali,” alisema Werema na kuongeza kuwa hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kulinda na kuheshimiwa kwa Dola, wakati wa kuendesha kesi mahakamani.
Alisema utaratibu huo ulikuwapo zamani, lakini ukaondolewa na aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi, Omari Mahita bila kufafanua sababu za kufanya hivyo.
--Rejea ya habari: Gazeti la HabariLeo