wavuti.weebly.com
  • Front
  • News blog
  • Scholarship links
  • Job links
  • Blog roll

Gharama mpya za huduma ya maji Dar

6/11/2009

 
Shirika la Maji Safi na Maji Taka (DAWASCO) limetangaza kupanda kwa bei mpya ya maji maeneo mbalimbali ya jiji la Dar Es Salaam. Afisa Uhusiano wa DAWASCO, Mary Lyimo, amesema kupanda kwa bei hizo ni kutokana na kanuni za hesabu za kurekebisha bei kwa kujumuisha mabadiliko na mwenendo wa kiuchumi na hali ya kiufundi ili kupambana na gharama za uendeshaji.

Maeneo yatakayokumbwa na gharama mpya:
  • Magomeni ambapo ujazo wa lita 36 awali ulikuwa ni sh 23,544 sasa ni sh 29,535
  • Kimara ujazo wa lita ulikuwa ni 36 kwa sh 23,544 bei mpya ni 29,535
  • Tabata lita 20 kwa sh 13,080 sasa ni sh 15,935
  • Temeke ujazo wa lita 43 kwa sh 28,122 sasa ni 35 kwa 28,685
  • Ilala ujazo uliokuwa ni lita 36 kwa sh 23,544 sasa ni 35 kwa sh 28,685
  • Katikati ya jiji ujazo ulikuwa lita 52 kwa sh 34,008 sasa ni 35 kwa sh 28,685
  • Kinondoni 43 kwa sh 28,122 sasa ni 45 kwa sh 37,185.
  • Kawe ujazo ulikuwa ni lita 52 kwa sh 34,008 sasa ni lita 41 kwa sh 33,785
  • Boko lita 52 kwa sh 34,008 sasa ni 41 kwa sh 33,785
  • Bagamoyo ilikuwa 31 kwa sh 20,274 na sasa ni 32 kwa sh 26, 135
Bei hizo zinaendana na masharti kama yalivyoainishwa katika kifungu namba 40.1 (a) cha mkataba wa ukodishaji na kupitia malengo ya kiutendaji yaliyoko kwenye mkataba wa ukodishaji kwa kiwango kilichoridhiwa na Mamlaka ya Udhibiti Huduma za Nishati na Maji (EWURA).

Mipango:
Ifikapo Januari 31, 2010 au kabla ya hapo, DAWASCO inatakiwa kuongeza idadi ya wateja waliofungiwa dira za maji kutoka 39,000 hadi 104,000 ambapo wateja wote wa Kimara, Kibaha, katikati ya jiji na Boko wanapaswa kuwa wamefungiwa dira za maji. “Na hii ni kupitia kanuni za utendaji kama ilivyoelekezwa kwenye kifungu namba 13 cha mkataba wa ukodishaji kati ya DAWASCO na DAWASA," amesema Mary.

Habari kwa mujibu wa gazeti DarLeo.co.tz

Comments are closed.
    Picture
    Get professional advise for a Tanzanian or UK visa. Contact T UK Visa consultancy, C: +255 222 139 502 or E: info@tukvisaconsultancy.co.tz

    Archives

    February 2014
    January 2014
    December 2013
    November 2013
    October 2013
    September 2013
    August 2013
    July 2013
    June 2013
    May 2013
    April 2013
    March 2013
    February 2013
    January 2013
    December 2012
    November 2012
    October 2012
    September 2012
    August 2012
    July 2012
    June 2012
    May 2012
    April 2012
    March 2012
    February 2012
    January 2012
    December 2011
    November 2011
    October 2011
    September 2011
    August 2011
    July 2011
    June 2011
    May 2011
    April 2011
    March 2011
    February 2011
    January 2011
    December 2010
    November 2010
    October 2010
    September 2010
    August 2010
    July 2010
    June 2010
    May 2010
    April 2010
    March 2010
    February 2010
    January 2010
    December 2009
    November 2009
    October 2009

    RSS Feed

    .
Powered by Create your own unique website with customizable templates.